Kuna somo ambalo liko wazi kabisa. Vikundi vyetu vingi hufanya hata zaidi ya maonyesho matano kwa wiki, na kupata mapato kiduchu, mara nyingine hata fedha ya usafiri kuwarudisha wanamuziki nyumbani baada ya onyesho haipatikani. Lakini tumeona kuwa maonyesho haya makubwa yaliyopangwa na kutayarishwa vizuri na pia kupewa promo ya kutosha huweza kuingiza kipato katika siku moja ambacho ni sawa na mapato ya miezi kadhaa ya vikundi vyetu katika mtindo wa sasa wa maonyesho ya kila siku yasiyo na matayarisho ya kutosha. Wanamuziki tutafakari!!!!!!!!!!!!!!
Sanaa na wasanii Tanzania
Blog ya picha na maelezo kuhusu vikundi na wanamuziki mbalimbali katika kazi zao
Wednesday, June 19, 2013
Tuesday, June 18, 2013
SAIDA KAROLI ASEMA SINA MPANGO WA KUFA BADO
![]() |
| SAIDA VERY |
Baada ya taarifa kuzushwa kuwa Saida Karoli amefariki katika
ajali ya meli habari za uhakika ni kuwa Saida Karoli wala hayuko mahala popote
jirani na Ziwa Victoria. Baada ya
kuweko Dar es Salaam wiki iliyopita, Saida na kundi lake walikodishwa na
kuelekea Makongorosi Chunya mahala aliko mpaka asubuhi hii. Saida Karoli
anasema hana mpango wowote wa kufa KARIBUNI.
MUNGU AMUONGEZEE SIKU NYINGI ZENYE FARAJA KATIKA MAISHA YAKE
HABARI ZIMEENEA KUWA INAHOFIWA SAIDA KAROLI AMEFARIKI DUNIA
Kutokana na maelezo kutoka blog mbalimbali ikiwemo Mjengwa Blog na Sundayshomary.com mwanadada muimbaji aliyekuwa kipenzi cha Watanzania mara baada ya kutoa wimbo wake Chambua kama karanga, Bi Saida Karoli amefariki dunia baada ya chombo alichokuwa akisafiria kutoka kisiwa cha Goziba kuzama baada ya kupigwa na dhoruba kubwa. Bado habari zaidi hazijapatikana hivyo tunasubiri habari za ziada na kuweza kuwapasha wapenzi wa mwanadada huyu.Friday, June 14, 2013
Thursday, June 13, 2013
LANGA KILEWO AFARIKI DUNIA
Msanii mwingine wa Hiphop Langa Kilewo ayelianza kujulikana
katika kundi la Wakilisha akiwa na Witness na Shaa amefariki dunia mchana huu.
Taarifa za Langa kuwa amelazwa hospitali zilianza kujulikana mapema leo katika
blog kadhaa zenye kufuatilia wasanii, zikieleza kuwa kalazwa kwa tatizo la malaria. Langa ambae aliwahi kukiri hadharani kuwa
ana tatizo kubwa la madawa ya kulevya na kutangaza kuwa ameachana na madawa
hayo kutokana na matatizo yaliyokuwa yanamletea. Hivi karibuni kama wiki mbili zilizopita, Langa
alikuwa akihojiwa katika kipindi cha Friday Night Live cha EATV akawa akimuongelea marehemu Ngwear na kumsifu
sana kuwa alikuwa na roho safi, pia Langa alikuwa anaelezea mipango yake ya baadae baada ya
kutoa video yake mpya aliyoifanya na P Funk na Fid Q iliyokuwa ikiitwa Rafiki
wa kweli. Alikuwa akiongelea kukamilisha video zake nyingine mbili ili kutoa
album mwishoni mwa mwaka. Hayatakuwa.
MUNGU AMLAZE LANGA KILEWO PEMA PEPONI
Wednesday, June 12, 2013
Subscribe to:
Posts (Atom)





