MCHORA VIBONZO ASOTA KIZUIZINI TOKA SEPTEMBA

Mchoraji Ramón Esono Ebalé
Cartoonists Rights Network International (CRNI) imemchagua mchora vibonzo. Ramón Esono Ebalé ambaye kwa sasa  yuko kizuizini Equatorial Guinea kuwa mshindi wa tuzo la  ’2017 Courage in Cartooning Award.’
CRNI kimesema kuwa kuchaguliwa kwa Ramon kumetokana na ‘Kuendelea kwake kukataa kutishwa , na ujasiri wake  dhidi ya selikali dhalimu’.
Joel Pett, Rais wa Bodi ya wakurugenzi ya ya CRNI alisema ‘ Ramón Esono Ebalé ni mzaliwa wa Equatorial Guinea ambaye kwa muda mrefu alikuwa akiishii Paraguay,’ 
Tuzo la ujasiri la  Award for Courage in Editorial Cartooning ni kengele ya kila mwaka inayotolewa kwa wachora vibonzo walioonyesha ujasiri na  kujitoa katika kuendeleza fani yao na kutetea uhuru wa kujieleza. 
Ramon alikamatwa tarehe 16 Septemba 2017 na vyombo vya usalama katika mji wa Malabo mji mkuu wa Equatorial Guinea. Kama ilivyosemwa hapo awali, Ramon alikuwa anaishi nje ya nchi na alikuwa karudi kwao kupata hati mpya ya kusafiria. Picha za mchoraji huyu mara nyingi zilikuwa zikimuongelea Rais na watumishi wengine wa serikali, kulikuwa na wasi wasi kuwa akikamatwa atashtakiwa kwa kosa la kukashifu viongozi, lakini amefunguliwa mashtaka ya kutakatisha pesa. Makosa ambayo CRNI inadai ni ya kutunga.
Tuzo lilikabidhiwa kwa Ramon japo kuwa hakuweko, wakati wa mkutano mkuu wa Association of American Editorial Cartoonists, uliofanyika siku ya tarehe 4 Novemba 2017 Hofstra University campus, Long Island, New York. Tayari maelfu ya watu wamekwisha tia saini maombi ya kuachiwa kwake, na hasa wakidai kuwa  sheria ya nchi hiyo hairuhusu mtu kuwekwa kizuizini zaidi ya masaa 72 kabla hajafunguliwa mashtaka. Mashirika ya kupigania haki za binadamu ya International rights group na Human Rights Watch (HRW) yamejaribu kuwasiliana na Rais wa nchi hiyo President Teodoro Obiang Nguema, kumuomba kumuachia mchora vibonzo huyo na kufuata matakwa ya sheria ya nchi hiyo.

Comments