WALUGULU ORIGINAL...GFC Musica Band















Walugulu Original, ndivyo inavyojiiita bendi ya GFC Musica. Bendi hii niliikuta ikiwa kazini katika ukumbi wa Chilakale baada ya kuelekezwa na rafiki zangu wa Facebook kuhusu kazi nzuri wanayoifanya, ni wazi pamoja na upya wa Bendi hii ikiwa watashikilia miiko ya ujenzi mzuri wa bendi hakuna sababu kwanini wasiweze kuwa katika bendi maarufu Tanzania, na kuirudisha Morogoro kwenye nafasi yake katika uwanda wa muziki wa dansi Tanzania.
Bendi nyingi zimechukua mfumo wa muziki wa Kikongo wa kupiga sebene na pia kuwa na wacheza show wengi na hivi ndivyo ilivyo kwa bendi hii. Kwa hiyo imeingia katika mashindano ya kutafuta nafasi ya kung’ara katika mtindo huo, kwa vile bendi ina vyombo vipya vizuri, wanamuziki wachanga wanaoonekana wana ari ya kufanya kazi, na pia wana mlezi ambaye ana nia ya kuona bendi inapata mafanikio, na pia kwa vile wasanii wanauwezo mkubwa, hakuna sababu yoyote kwanini hawataweza kuleta upinzani kwa bendi kubwa ambazo zimekwisha ota mizizi kama, Twanga Pepeta, Extra Bongo na kadhalika.

Comments

Anonymous said…
gfc ipo juu sana wakaze buti kwa kweli