HAKIMILIKI NI NINI? msanii jielewe


HAKIMILIKI KWA UFUPI SANA

Hakimiliki ni nini?
Hakimiliki ni haki za kisheria anazopewa mtunzi na mbunifu katika kazi zake za utunzi na ubunifu. Hakimiliki huambatana na haki nyingine zinazoitwa Hakishiriki ambazo hulinda wale ambao huwezesha kufanikiwa kwa kazi za hakimiliki huonekana hadharani. Kama ni mchezo wa filamu waigizaji hulindwa na Hakishiriki wakati mtunzi wa script hulindwa na hakimiliki, katika muziki, Producers hulindwa na Hakishiriki mtunzi wa wimbo hulindwa na Hakimiliki, pia haki hizi huvilinda vyombo vya utangazaji katika haki za vipindi vyao.
Hakimiliki hulinda aina nyingi za kazi kama vile;
a.     Kazi za kimaandishi (vitabu,hotuba,magazeti,novo, hadithi fupi na ndefu, mashahiri na kadhalika)
b.     Kazi za muziki (tungo za muziki zenye maneno na ala tupu, mashahiri ya muziki, ringtones za simu na kadhalika
c.     Kazi za kisanii (michoro, vibonzo, picha za rangi za maji, fotografia, za kuchonga, ufinyanzi, ususi na kadhalika)
d.     Sanaa za maonyesho (Michezo ya kuigiza ya jukwaani,operas na kadhalika)
e.     Filamu na kazi nyingine za multimedia (video, video games,vipindi vya TV,cartoons, filamu nk)
f.      Program za kompyuta.
Kwa maelezo ya hapo juu utaweza kuona kuona kuwa si kila msanii hulindwa na Hakimiliki, wengine haki zao zinalindwa na Hakishiriki.

Hakimiliki hutoa haki za aina mbili.
i.               Moral rights- Haki za kimaadili ambazo hulazimisha watumiaji kumtambua mtunzi katika kazi zake, kwa mfano mtunzi wa kitabu kutajwa kwenye jalada la kitabu, au mcheza filamu kutajwa jina lake mwisho au mwanzo wa filamu. Hki hizi huwezi kumpa mtu mwingine.
ii.             Economic rights- hizi ni haki zinazoleta faida za kiuchumi katika kazi ya mtunzi, na hizi ndio huleta migogoro na kelele nyingi tunazozisikia kila siku kuhusu wasanii kuibiwa.


Economic rights- Hizi ndizo haki ambazo huvunjwa sana na huonekana sana matokeo kwani huwatajirisha wengine na wengine kuwatia umasikini. Haki hizi hutolewa kwa mtunzi pekee (exclusive rights) na hivyo yeye huweza kuzitumia kwa njia ambayo anaweza kuona inafaa katika kumuongezea kipato. Haki hizi ni kama zifuatazo;
i.               kurudufu…kutengeneza nakala ambazo anaweza kuuza
ii.             kutafsiri kazi
iii.           kubadili matumizi ya kazi (km wimbo wa dansi kugeuzwa ringtone, kitabu cha hadithi kuwa sinema na kadhalika)
iv.            Kuonyesha hadharani kazi (Exhibition au performance)
v.              Kusambaza kazi…kuuza kazi
vi.            Kutangaza katika vyombo vya utangazaji(Broadcasting)
vii.          Mawasiliano ya kazi (kwa kupitia intanet)
Mtunzi hukabidhi haki hizi kwa wasambazaji, ili wasambaze kazi zake kwa makubaliano maalum, pasipokuweko na makubaliano hapo ndipo wizi wa kazi za sanaa kwa njia ya Piracy hutendeka.
 Kutokana na mapato makubwa ambayo yanaweza kutokana na mapato ya Hakimiliki, kwa watunzi na serikali, serikali pamoja na kuunda sheria za hakimiliki huwa na ofisi ya serikali ya kuratibu uendeshwaji wa sera na shughuli za hakimiliki,  hivyo ni muhimu kuwa na COPYRIGHT OFFICE (Tanzania hatuna), ambayo yenyewe huratibu vyombo mbalimbali vinavyohusika kwa njia moja au nyingine katika Hakimiliki.
Ili kulinda haki za wasanii wa muziki na filamu huwa kunakuweko vyama vya wadau vya hakimiliki, huwa kunakuweko na Performing Rights Societies ambazo hufuatilia matumizi ya hakimiliki kwa mfano katika matumizi kwenye Radio, TV, kumbi mbalimbali nakadhalika, halafu huweko Mechanical Rights Societies ambazo hufuatilia taratibu za mauzo ya kazi za sanaa.
Katika nchi yetu, Hakimiliki hulindwa kwa maisha yote ya mtunzi na miaka hamsini baada ya kifo chake. Kwa ulinzi huu mrefu, kila mara wanaouza masters waelewe wanauza pamoja haki hii, ambayo ingewawezesha watoto wao na wajukuu zao kufaidi matunda yao. Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kuna wakulima wanakula mpaka mbegu……
25

Comments

kazi nzuri kaka! Lakini nasikitika ni wasanii wangapi watabahatika kupata elimu kama hii. Nashukuru kwa kuwa nimefika kwenye blogu yako na sijatoka bure. kwani mimi pia ni msanii na ukweli nimejifunza jambo.Ombi langu makala hizi ziombee gazetini na kwenye radio pia.