BURUDANI IJUMAA YA LEO

Leo imekuwa siku ya kuzunguka katika sehemu mbalimbali, nilianzia Sinza katika Bar ya T Garden ambapo kulikuweko na bendi inayoongozwa na mpiga bezi wa zamani wa Sikinde Mzee Julius Mzelu- JM MBETA BAND
Fred Mzelu

Julius Mzelu

Nikatoka hapo na kuenda kuangalia mashindano ya Miss Ilala, sikukaa sana maana kwa kweli vyombo vilivyotumika kwa sauti viliipunguza utamu show ile, niliona alfu ishirini yangu imeenda kama sadaka. Nikapita Mango Garden ambako niliwakuta Akudo Band wakiwa na muimbaji wao mpya anayejitambulisha kwa jina la 'Lialia'










Hatimae nikapita Mashujaa muzika na kumkuta Charlz Baba na kundi lake katika ukumbi wa Business maeneo ya Victoria




Comments

Stiba said…
Ziara yako imetulia anko Kitime, umetupatia overview nzuri ya burudani za bendi zetu! Ahsante!
Rachel Siwa said…
Kwenye pitapita zoote hizo wapi ulipata Burudani ya uhakika?
jfk said…
Rachel, ajabu ni kuwa mahala ambapo muziki ulikuwa bure ndipo nilipoburudika zaidi, kwenye bendi ya Mzelu.