Salamu toka kwa Nguza



 
Nimekwenda gereza la Ukonga asubuhi hii kumsalimia Nguza na mwanae Papii, nimewakuta wachangamfu wenye afya nzuri. Nguza kanituma NIWASALIMIE WOTE, naomba nitumie jukwaa hili kutangaza salamu hizo. Ni wazi italazimika kuomba muda wa ziada kutoka kwa uongozi wa Magereza kuzungumza zaidi na Nguza, jambo mojawapo ambalo tutalizungumza ni kuhusu mapato ya wimbo wa Seya. Pamoja na umaarufu wote ni jambo la kusikitisha kuwa Nguza anasema hajapata fedha yoyote kutoka wimbo ule, zaidi ya fedha alizopewa kuingia studio kuurekodi. Swali ni nani anazipokea fedha za wimbo ule?

Comments

A.J.MLANZI said…
mpe salam na kama kuna njia nyingine ya kuuza nyimbo yake ili aone mapato tujulishane apewe support.
Anonymous said…
Yaani Africa bwana sijuwi kwa nini wanamuziki wetu wananyonywa. Hili tatizo liko hata RDC na sehemu zingine hapa Africa. Mwanamuziki anajituma kwa kazi yake na jasho lake uliwa na wengine. Inaudhi na kusikitisha sana.