MALKIA VANESSA MDEE AFANYA KAZI NA MFALME PETER WA P SQUARE

Mara baada ya kumaliza kushiriki kuigiza kwa mara ya kwanza katika katika tamthiliya  ya MTV, inayoitwa SHUGA,Vanessa Mdee ameachia wimbo wake mpya unaoitwa Kisela. Katika tamthiliya hiyo ya SHUGA, Vanessa ameshirikiana na waigizaji wa Afrika Kusini  kama  Nick Mutuma and Emmanuel Ikubese. Na katika wimbo huo mpya Vanessa ameshirikiana na Mfalme wa Pop wa Nigeria Mr P  au Peter Okoye wa PSquare, hakika ni mambo ya kusifika. Wimbo huu wenye vyombo vya upepo vya nguvu, unaongelea hadithi ya mwanamke analalamika anavyotendwa na mpenzi wake, anaeendesha mapenza Kisela, Producer wa wimbo huu ni Mnaijeria producer EKelly, ambaye ana nyimbo nyingi ambazo zimefanya vizuri sana Afrika, producer huyu ndie aliutengeneza wimbo wa VeeMoney wa Cash Madame. Video ya wimbo imeongozwa na Clarence Peters, na hakika Peter Okoye na Vanessa wameonyesha ukomavu wao katika sana, na kazi hii inaonyesha hasa kwanini wao ni Mastaa.
Vanessa  alimsifia Peter  kwa kuonyesha hasa nini maana mwanamuziki ambaye ni star , na anaona kama ni ndoto ilikuja kuwa kweli kushirikiana naye, pia alisifu kuwa Peter amempa sio tu somo katika muziki na utoaji wa burudani, lakini pia somo la umahiri katika kazi na unyenyekevu kwa wengine.


Comments