MPIGA BASS GUITAR WA TOT AFARIKI BAADA YA AJALI YA PIKIPIKI



Samwel Mshana maarufu kama Mshana Bass, aliyekuwa mpiga gitaa la bezi katika kundi la TOT  amefariki dunia leo alfajiri. Samwel alikuwa amelazwa hospitali baada ya ajali, ambapo pikipiki aliyokuwa akiendesha iligongana na bajaji maeneo ya Mwananyamala Komakoma. Kifo chake kimekuwa cha ghafla na kushangaza kwa kuwa kwanza ajali haikutokea kwenye mwendo kasi na baada ya ajali hakuonekana kuwa na majeraha yoyote makubwa, na hata siku ambazo rafiki zake walikuwa wakimtembelea hospitali hakuonyesha dalili kuwa ni jambo kubwa. Kazi ya Mungu haina makosa.
 Mungu amlaze pema SAMWEL  MSHANA

Comments