MCHEKESHAJI NAIJERIA AINGIA MKATABA WA DOLA MILIONI 1


Lagos, Nigeria, Henry Obiefule mchekeshaji maarufu kutoka Nijeria atacheka sana mwaka huu baada ya kupata mkataba uliompatia dola milioni 1 za Kimarekani, (shilingi za Kitanzania zaidi ya 2,000,000,000/-). Hii ni baada ya kuteuliwa kuwa balozi wa  Vomoz Communications, au kwa Kiingereza kuwa Brand Ambassador wa Vomoz Communication.

Obiefule anaejulikana zaidi kama  Chief Obi, ni maarufu kwa kuigiza tabia za wazazi wa kawaida wa Kinaijeria. Historia fupi ya Obiefule, ni kuwa alianza kutengeneza video fupi kupitia mtandao wa Keek akahamia Vine na hatimae Instagrama alipojikuta ana followers laki mbili. Tayari ameshashiriki katika video za muziki za 2Face, Olamide na jidenha.


Comments