Mkataba wa Kumkodi Mwanamuziki au Mwimbaji Msindikizaji Kwa ajili ya kurekodi

Ni jambo la kawaida kabisa kuona makubaliano makubwa katika tasnia ya muziki Tanzania yanafanywa bila mikataba bali kwa makubaliano ya mdomo. Hili ni tatizo ambalo lazima lirekebishwe, kwani linaleta hasara kubwa kwa wasanii kutokupata haki zao stahili na mara nyingine kudhulumiwa kabisa. Hivyo basi kwa kuwa mikataba ya muziki huwa na lugha ngumu ifuatayo ni mikataba mabayo imerahisishwa na UNESCO ili wanamuziki waweze kuitumia kwa marekibisho kidogo kutegemeana na hali halisi. Hii ni mifano ya mikataba ambayo hutumika dunia nzima. Usikubali kuanza kazi bila mkataba wa maandishi…. JE UNATAKIWA KUFANYA KAZI YA MUZIKI KWENYE ALBUM YA MTU MWINGINE? MKATABA HUU HAPA  
 
 Mkataba wa kumkodi Mwanamuziki au Mwimbaji Msindikizaji Kwa ajili ya kurekodi Santuri 

 Mkataba unaeleza masharti ya kumkodi mwanamuziki au mwimbaji msindikizaji kwa ajili ya kurekodi santuri moja au zaidi zitakazotayarishwa kibiashara. Mkataba unaainisha wajibu wa mtayarishaji na vilevile ule wa wanamuziki na waimbaji.

 MWANAMUZIKI AU MWIMBAJI MSINDIKIZAJI MTAYARISHAJI WA SANTURI 
 KIFUNGU CHA 1 – Madhumuni.  
Mtayarishaji anamkodi mwanamuziki au mwimbaji msindikizaji katika nafasi yake ya kitaalamu kurekodi santuri moja au kadhaa. Santuri zitatumiwa mojamoja au kama sehemu ya Albamu. Mkataba lazima ujazwe kikamilifu pale inapobidi, kwa kuzigatia masharti ya sheria za kazi za nchi ambazo mkataba unasainiwa. 
 KIFUNGU CHA 2 – uidhinishaji wa Matumizi. MWANAMUZIKi au MWIMBAJI MSINDIKIZAJI anaidhinisha upangiliaji wa maonesho yake na kurudufu santuri zilizoainishwa kwenye kifungu cha 1 na vile vile kufanya biashara ya santuri hizo kwa umma. Hivyo mtayarishaji atakuwa na haki ya kuzalisha, kuchapisha, kusambaza itakuvyokuwa kuuza kwenye kibebeo cha aina yoyote ( K7, CD, DVD ya sauti au muundo wowote wa siku zijazo nk ) au kwa mawasiliano ya mtandao (Intaneti na mingineyo), kutangaza katika muundo wowote, chini ya kichwa cha habari, nembo au alama ya chaguo lake na duniani kote, santuri zilizoanishwa katika kifungu cha 1. Unufaikaji wowote zaidi ya matumizi yaliyoelezwa hapo juu, yakiwamo matumizi kwa ajili ya matangazo ya biashara, matumizi ya kielimu, matumizi katika sinema au onesho, na matumizi kwenye bidhaa maalumu, yatahitaji kwanza kupata idhini ya asasi ya usimamizi wa pamoja inayosimamia haki za wanamuziki na waimbaji wasindikizaji. Ili kuruhusu matumizi sahihi ya haki. Mtayarishaji anawajibika kuhakikisha mwanamuziki au mwimbaji msindikizaji anasaini karatasi ya kurekodi kipindi kulingana na taratibu za kitaalamu, na kuwasilisha nakala ya karatasi hii ya kurekodi kipindi kwenye asasi ya usimamizi wa pamoja ambayo inasimamia haki za wanamuziki na waimbaji wasindikizaji katika nchi zilizotarishwa santuri. Zaidi ya hayo msanii anaridhia matumizi ya jina na picha yake, kama vitahitajika, kuhusiana na matumizi ya santuri hizo. 
 KIFUNGU CHA 3 – Wajibu wa mtayarishaji. MTAYARISHAJI anajukumu la kuheshimu wajibu wote uliowekwa na sheria za kijamii kuhusiana na kumkodi MWANAMUZIKI au MWIMBAJI MSINDIKIZAJI. Mtayarishaji anawajibika kumlipa mwanamuziki au mwimbaji msindikizaji kiasi cha _____________________ kwa kila kipindi cha kurekodi, ili kufidia kushiriki kwake katika kurekodi santuri, na vilevile kwa ajili ya uchapishaji na mauzo ya miziki kwenye aina yoyote ya kibebeo (K7, CD, DVD ya sauti n.k) au katika mawasiliano ya mitandao (Intaneti au mingineyo). Upigaji wa santuri katika utangazaji utatakiwa kuliipiwa moja kwa moja na mashirika ya utangazaji kwenye asasi ya usimamizi wa pamoja ambayo inasimamia haki za wanamuziki na waimbaji wasindikizaji katika nchi matangazo yanamotolewa. 
 KIFUNGU CHA 4 – wajibu wa Mwanamuziki au Mwimbaji Msindikizaji. 
Mwanamuziki kutoka nje au mwimbaji msindikizaji kutoka nje ya nchi anahakikisha kuwa amepewa kibali cha kufanya kazi kwenye nchi santuri zinapotayarishwa na kuwasilisha uthibitisho wa jambo hilo. Mwanamuziki au mwimbaji msindikizaji anawajibika kuwepo kuanzia ___________________ hadi
___________________katika sehemu ifuatayo _____________________ kushiliki katika vipindi vya kurekodi ambavyo vitafanyika kulingana na ratiba zifuatazo:- ______________________________________________________________________________ Kifungu cha 5 – mambo mbalimbali  
Mkataba huu unaongozwa na sheria ya nchi unamofanyika utayarishaji. 
Umesainiwa (mji)…………………………………….. Tarehe ……………….. Katika ……………… nakala halisi. 
 MWANAMUZIKI AU MWIMBAJI MSINDIKIZAJI ________________________________________________________________________   MTAYARISHAJI ________________________________________________________________________  

Comments