RATIBA YA MSIBA WA MAREHEMU SALOME KIWAYA


Taarifa ya ratiba ya msiba wa marehemu Salome Kiwaya aliyekuwa Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Dodoma na mwanamuziki, aliyefariki jana 07/10/2016, kwa ajali ya gari maeneo ya Kilimo Kwanza Dodoma Mjini. Msiba uko nyumbani kwa marehemu Mtaa wa Image, Kata ya Kilimani, Wilaya ya Dodoma Mjini. RATIBA:

 1.Tarehe 08/10/2016 - maombolezo  yanaendelea nyumbani Image Kilimani Dodoma.

2.Tarehe 09/10/2016 kuanzia saa 2:00 asubuhi - mwili wa marehemu utaletwa nyumbani kutoka  chumba cha maiti cha General Hospital Dodoma.

3. Tarehe 09/10/2016 saa kuanzia 6:00 mchana -salamu mbalimbali za Viongozi na Makundi Maalumu zitaanza kutolewa.

Saa 8: 00 mchana- mwili wa marehemu utatolewa nyumbani, na kuelekea Kanisa Kuu Roman Catholic. Baada ya Misa, msafara wa mwili wa marehemu utaelekea Kijiji cha Mtila, Kata ya Matola Mkoa wa Njombe kwa ajili ya maziko tarehe 10/10/2016 siku ya Jumatatu.




Comments