JOHN KITIME NDIE KATIBU MKUU MPYA WA SHIRIKISHO LA MUZIKI TANZANIA

-->

John Kitime Katibu Mkuu Shirikisho la Muziki Tanzania
Rais wa Shirikisho la Muziki Tanzania leo amemtangaza John Kitime kuwa Katibu Mkuu wa Shirikisho hilo. Uchaguzi Mkuu wa Shirikisho hilo ulifanyika mwezi wa pili na vyam 8 vya Shirikisho hilo kuchagua viongozi wake. Nafasi ya Katibu Mkuu ilikuwa wazi. John Kitime ni mwanamuziki wa bendi ya Kilimanjaro (Wananjenje), ambaye miaka ya 90 alikuwa Mwenyekiti wa CHAMUDATA na wakati huo chama kilikuwa katika ufanisi mkubwa wa kuweza hata kuwa na ushirikiano na mashirika ya miasaada ya nje yaliyowezesha chama hicho kupata misaada mbalimbali, na hata kufanya matamasha makubwa ya muziki. Pia Kitime ni Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanamuziki chama ambacho pia kimewezesha wanacham wake kupata bima ya Afya. Kwenye mkutano na waandishi wa habari, Katibu Mkuu huyo alisema  kati ya mambo atakayoanza nayo ni kuimarisha Shirikisho kwa kuimarisha vyama wanachama wa Shirikisho, ikiwemo kuhamasisha kuanzishwa vyama vingine. Kuonyesha kuwa anania ya kutekeleza hizo mwisho wa mkutano huo aliwahamasisha waandishi wa habari za muziki kuanzisha chama chao. Vyama vilivyo wanachama wa Shirikisho la Muziki Tanzania ni Chama cha Muziki wa Dansi Tanzania CHAMUDATA, Chama cha Muziki wa Rumba CHAMURUMBA, Chama Cha Muziki wa Injili Tanzania CHAMUITA, Tanzania Folk Music Development Association TAFOMUDEA, Tanzania taarab Association TTA, Tanzania Urban Music Association TUMA   

Comments