WAZIRI WA HABARI UTAMADUNI SANAA NA MICHEZO KUKUTANA NA WANAMUZIKI JUMATATU

KATIKA hatua ya kujua mafanikio na changamoto za muziki wa dansi na hatimae kupanga yajayo, Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo atakutana na wanamuziki wa Dar es Salaam katika ukumbi wa Vijana Social Hall Kinondoni siku ya Jumatatu kuanzia saa nne asubuhi. Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa miaka mingi kwa Waziri wa Utamaduni kufanya mkutano wa namna hii na wanamuziki.

Comments