WAPENZI WA KUNDI LA TAARAB LA WASHAWASHA CLASSIC WAMSAPRAIZ MPIGA KINANDA WAO

WADAU mbaimbali wa muziki, Jumapili iliyopita 24/1/2016, walilitumia jukwaa la bendi ya taarab ya Washawasha Classic, kumfanyia mwimbaji nyota wa bendi hiyo, Omary Sosha, sherehe ya kushitukiza ya siku yake ya kuzaliwa.
Tukio hilo la kusisimua na ambalo liliteka hisia za wengi, lilifanyika ndani ya ukumbi wa Centre Grill ‘Flamingo’ ambapo Washawasha Classic iliyo chini ya mpapasa kinanda mahiri, Amour Maguru, ilikuwa ikitumbuiza.
Wakati burudani ya muziki ikiendelea, ghafla liliibuka kundi la wadau kadhaa maarufu, wakiwemo ‘2po Dar Crew’, ‘Team Mombasa Raha’, ‘Mbaine Company Group’ wakiongozwa na wasanii Hummer Q na H Mbizo.
Walipoingia, wadau hao waliokuwa na keki kubwa na zawadi nyingine kemkemu, walikwenda moja kwa moja jukwaani ambako sosha alikuwa akipagawisha mashabiki kwa kuimba, wakamvamia na kuanza kumpongeza kwa wimbo wa ‘happy birth day’.
Alipohojiwa na mwandishi wetu baada ya tukio hilo, Sosha alisema anafurahi kuona wadau na wasanii wenzake wametambua umuhimu wa siku yake ya kuzaliwa, ambapo kwa upande mwingine ameahidi kuzidi kuwanao bega kwa bega kiburudani.

Comments