Kundi la Muziki la Navy Kenzo Lashika Namba Nne Katika Video 50 Zilizobamba Zaidi MTV Base Mwaka 2015


Kundi la muziki la Navy Kenzo linaloundwa na Aika na Nahreel wamefanya vizuri baada ya video ya wimbo wao wa Game, waliomshirikisha Vanessa Mdee kushika Namba Nne katika chart ya Video 50 Bora za MTV Base Africa zilizofanya vizuri mwaka 2015..
Diamond Platnumz na wimbo wake wa Nana umeshika namba 5 katika chart hizo, wimbo huo wa Nana pia umetengenezwa na Producer Nahreel, kitu kinachomfanya aendelee kuwa producer bora zaidi kutoka Tanzania na Afrika ya Mashariki kwa ujumla,
Mwimbaji Wizkid wa Naigeria ameshika namba 6.
Pongezi ziende kwao @nahreel,@aikanavykenzo wanaounda Kundi la Navykenzo
Pia pongezi kwa Diamond Platnumz kwa kuwa namba 5 katika chart hiyo...

Comments