FILAMU YA SINGELI KUFWATIWA NA JICHO LA MCHAWI

IKIWA ni wiki tatu tangu iachiwe, muviya ‘Singeli’ imeonekana kufanya vema sokoni kiasi cha kufunika nyingine zilizotangulia.
Kwa mujibu wa waandaji wa filamu hiyo, Mmaka Film Production, kopi za awali zimemalizika na sasa wameanza kazi ya kudurufu nyingine ikiwa ni maombi maalum ya wateja wao.
“Tunashukuru kuona muvi hii ya ‘Singeli’ inaendelea kufanya vyema sokoni na mashabiki nchini wanaonekana kuipokea kwa mikono miwili,” alisema Mkurugenzi wa Mmaka Film, Omary Mmaka.
Mmaka alisema kuwa, hivi sasa wapo katika maandalizi ya kazi yao mpya inayokwenda kwa jina la ‘Jicho la Mchawi’, ambayo nayo itashirikisha nyota wengi wenye majina kama ilivyokuwa kwenye ‘Singeli’.

Comments