SIMON MWAKIFWAMBA APATA AJALI MOROGORO

Rais wa Shirikisho La Filamu Tanzania (TAFF), Mwakifwamba Simon, amepata ajali ya gari karibu na Mkundi, nje kidogo ya mji wa Morogoro karibu na mizani, usiku huu wakati akitoka Dodoma kuja Dar es Salaam. Gari aliyokuwa akiiendesha aina ya Toyota Noah T 176 CYM mali ya TAFF imepinduka na kuharibika vibaya, lakini yeye yuko salama. Kwa kadri ya maelezo ya Mwakifamba ni kuwa alipokata kona ghafla mbele akaona pikipiki ambayo haikuwa na taa wala reflector na katika kuikwepa na kuingia pembeni ya barabara tairi mbili zilipata pancha na gari kupinduka. Hakuna aliyeumia katika ajali hiyo. Mpaka tunapata taarifa hii alikuwa bado Morogoro akiandika maelezo kwenye kituo cha usalama barabarani.

Comments