KHAMIS AMIGOLAS KUZIKWA KESHO MAKABURI YA KISUTU


RIP Amigolasy
KHAMIS AMIGOLAS  wanamuziki wa miaka mingi aliyepitia bendi kadhaa zikiwemo African Beat, African Stars na hatimae Ruvu Stars amefariki dunia jana usiku kutokana na ugonjwa wa moyo ambao wanaomfahamu wanasema ulikuwa ukimsumbua kwa miaka mingi. Khamis aliyefahamika sana kwa mustachi wake alikuwa mwanamuziki muimbaji mtulivu na mcheshi, mwenye kupenda utani sana.  Msiba uko jirani na shule ya Msingi ya Mianzini Mburahati. 
Mpaka sasa jamaa wa karibu wametaarifu kuwa mazishi yatakuwa kesho Jumatatu mchana katika makaburi ya Kisutu,
Mungu ailaze pema peponi roho yake Amin

Comments