FILAMU YA KUTAKAPOKUCHA JOHN KITIME NA MZEE MAGALI NDANI

ILE  muvi ambayo mwanamuziki John Kitime alishiriki akiwa na wasanii wengine wakongwe akiwemo mzee Magali na waalimu mahiri wa sanaa kutoka TASUBA, hatimae itakuwa dukani 24 november 2014, ikisambazwa na kampuni ya Proin Promotions Ltd. Filamu hii ilikuwa iwe dukani mwezi June lakini ikasubirishwa ili kufanyiwa editing zaidi.Katika filamu hii, John Kitime ni Mwenyekiti wa kijiji anaejiona Nusu Mungu na hasa pale ambapo mwanae , ambae ni mpiga karate mashuhuri anapoingia Kijijini na kutisha watu kwa kupiga watu hovyo hapo Kijijini. Mzee magali na mwanakijiji ambaye amepata elimu na anaweza kuzungumza Kiingereza jambo ambalo mwenyekiti wa Kijiji anaona ni tatizo kwani anaweza kunyang'anywa uongozi na msomi huyu. Ni picha yenye vituko, vichekesho, na muziki unaopigwa na gitaa na yeye Kitime. Hadithi imeandikwa na Irene Sanga. Angalia picha za utengenezaji wa muvi hii.




Comments