ILE muvi ambayo mwanamuziki John Kitime alishiriki akiwa na wasanii
wengine wakongwe akiwemo mzee Magali na waalimu mahiri wa sanaa kutoka
TASUBA, hatimae itakuwa dukani 24 november 2014, ikisambazwa na kampuni
ya Proin Promotions Ltd. Filamu hii ilikuwa iwe dukani mwezi June lakini
ikasubirishwa ili kufanyiwa editing zaidi.Katika filamu hii,
John Kitime ni Mwenyekiti wa kijiji anaejiona Nusu Mungu na hasa pale
ambapo mwanae , ambae ni mpiga karate mashuhuri anapoingia Kijijini na
kutisha watu kwa kupiga watu hovyo hapo Kijijini. Mzee magali na
mwanakijiji ambaye amepata elimu na anaweza kuzungumza Kiingereza jambo
ambalo mwenyekiti wa Kijiji anaona ni tatizo kwani anaweza kunyang'anywa
uongozi na msomi huyu. Ni picha yenye vituko, vichekesho, na muziki
unaopigwa na gitaa na yeye Kitime. Hadithi imeandikwa na Irene Sanga.
Angalia picha za utengenezaji wa muvi hii.
Comments