TALENT BAND YA HUSSEIN JUMBE IKIBURUDISHA KISUMA SABASABA MBAGALA

BENDI ya Talent inayoongozwa na mwanamuziki nguli Hussein Jumbe, imeendelea kutesa kwenye kiwanja chake cha nyumbani, Kisuma Sabasaba, Mbagala, jijini Dar es Salaam walipokuwa wakitumbuiza, katika onesho lao la kawaida la kila wiki.
Mwandishi wa habari hizi aliyekuwamo ndani ya ukumbi huo wa Kisuma, alishuhudia namna mashabiki walivyokuwa wakivisusa viti vyao mara kwa mara na kujimwaga katikati kucheza, huku baadhi yao wakionekana kupagawa zaidi na kutuza.
Jumbe mwenyewe alikuwa akiwakosha zaidi mashabiki wake kwa kuwafyatulia vibao vyake vikali, huku vingine vikiwa ni vile alivyovirekodi alipokuwa katika bendi za Mlimani Park Sikinde na Msondo Ngoma Music.
Onesho hilo lilimalizika majira ya saa 7:00 usiku, huku wapenzi na mashabiki mashabiki wakipiga kelele wakiomba rhumba liendelee kutokana na kuwa bado wana hamu ya kuendelea kuusakata muziki wa Talent.


                           Picha za Wana Talent Band jukwaani Kisuma Bar Mbagala










Comments