PATRICK KAMALEY ATUA EXCEL BAND

MKONGWE Patrick Kamalee akiwa na bendi yake mpya iitwayo Excel One, jana waliwasha moto mkali wa burudani katika kiwanja cha Kimboka Night Park, Buguruni, jijini Dar es Salaam na kukosha vilivyo nyoyo za mashabiki.
Kama kawaida, musicintanzania ilikuwapo eneo la tukio na kuwa shuhuda wa kile kilichokuwa kinaendelea ambacho si kingine bali ni burudani pevu kutoka kwa baadhi ya wanamuziki nguli wa miondoko ya dansi.
Bendi ya Excel inatumbuiza zaidi vibao vya kukopi kutoka kwenye bendi nyingine ambazo kwa sasa hazipo katika ulimwengu wa muziki, ambapo nyimbo nyingi ni kutoka kwenye makundi aliyowahi kuyatumikia Kamalee.


PATRICK KAMALEY












Comments