NEW ADEN MODER TAARAB YACHIZISHA MTU MONNIE JUNCTION

WAKATI mwingine burudani ya muziki wa kiingilio kinywaji una raha yake, kama ilivyoshuhudiwa  katika ukumbi wa ukumbi wa Monnie Junction, jijini Dar es Salaam.
Katika ukumbi huo jana, kundi la mipasho la New Aden Modern Taarab lilikuwa likitumbuiza na kuonekana kukonga zaidi nafsi za mashabiki waliokuwa wamehudhuria shoo hiyo.
Baadhi ya picha hapo chini, mwanadada ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja alionekana kucharuka zaidi kila pale Wana Aden walipokuwa wakiporomosha nyimbo.
Aden ni kati ya makundi ya mipasho yaliyotapakaa kwa wingi hivi sasa, yanayofanya maonyesho yake kwa kurindimisha zaidi vibao vya kukopi; vya zamani na vinavyotamba sasa ambavyo vimerekodiwa na makundi mengine.
Hata hivyo, kundi hilo lililo chini ya Mkurugenzi wa Salum Haji Chaurembo, lina nyimbo zake kadhaa ambazo hazijabahatika kupata umaarufu kwa mashabiki kama vile ‘Sikwa Cheketu Cheketu’....YALIYOJIRI...









Comments