MSONDO NA TALENT BAND JUKWAA MOJA AGOSTI26

WAKALI wa Dansi, Talent Band chini ya Mkurugenzi Hussein Jumbe, Alhamisi Agosti 26, mwaka huu, wanatarajiwa kukutana uso kwa uso na kaka zao, Msondo Ngoma Music, kwenye uzinduzi wa ukumbi wa Kisuma Mwembeyanga, jijini Dar es Salaam.
Onesho hilo ni la kawaida, ambapo bendi hizo zimealikwa kutoa burudani kwenye shughuli hiyo ya uzinduzi wa ukumbi huo, lakini hata hivyo tayari baadhi ya mashabiki wa Talent na Msondo wameanza kuligeuza kuwa pambano.
Katika onesho hilo lililopangwa kuanza kuunguruma majira ya saa 12:00 jioni, bendi hizo zimejipanga kukonga nyoyo za mashabiki wao kwa kuwaporomoshea nyundo zao kali; mpya pamoja na zile zamani zinazoendelea kutesa hadi sasa. 

Comments