MPOKI UJERUMANI......

Msanii maarufu nchini Tanzania, Muarabu wa Dubai (a k a Mpoki), ametua katika Jiji la Frankfurt na kuelekea moja kwa moja katika jiji la maraha Aschaffenburg ambapo atalala usiku mmoja na kuendelea na safari siku ya pili  kuelekea   Berlin  ambapo atahudhuria mkutano mkuu wa Umoja wa watanzania Ujerumani (U T U), Kongamano la biashara pamoja na sherehe za Muungano wa Tanzania.

Mpoki alitua  katika uwanja wa kimataifa  wa Frankfurt mnamo saa 10:30 alasiri na ndege ya shirika la ndege la Ethiopia Airlines akitokea Dar es salaam kupitia Addis Ababa. Msanii huyo alipokelewa na mwenyekiti wa Watanzania nchini Ujerumani.


Comments