MAONI YA WACHAMBUZI KUHUSU MWENENDO WA MUZIKI WA DANSI NCHINI 2


Robbie Mwangata Asante sana kaka Sampu Mussa Sampu. Hata hivyo hapa kwetu nchini ukionekana unapenda au kuzungumzia muziki huu wa dance unaonekana kama umepitwa na wakati kitu ambacho mimi binafsi kinaniuma sana. Na kuna baadhi ya radio station hazina mpango kabisa na muziki huu. Kiuhalisia muziki huu watu wengi wanaukubali sana na kuupenda sana lakini kweli kabisa umekosa wawakilishi kila sehemu hapa nchini. Mbali na radio na Television ambazo zinawakilisha vema muziki huu lakini kuna Tv na Radio ambazo ukisikiliza wanavyouchambua muziki huu lazima utakasirika sana. kiufupi wengine hawaujui lakini wanafanya hivyohivyo kwa kuwa nadhani wamepangiwa au wenye radio na tv ni watu wao wa karibu. Kazi yangu kubwa ni udj na kwasasa utagundua kuwa hata bongo flavour na yenyewe wanataka kuwa kama dance. Maeneo mengi niliyokwenda kupiga muziki niliunganishwa na drums na kuna mtu anapiga drums kwenye kila wimbo nilioupiga. BINAFSI INANIUMA SANA.

Dakta Masomo Lupembe Genre yoyote ile ya muziki ni sawa na 'living entity' {kiumbe hai}, huzaliwa, hukua, hukomaa, huchoka, huzeeka na kisha {kama hakuna juhudi za kui-rejuvenate} inakufa! Sioni mkakati wowote wa kutaka kuunusuru muziki wa dansi; umeachwa ufe kimyakimya!


Mussa Ngayatu Fred mm nakubaliana na ww kwa asilimia 101% moja nkupa zawadi.Mm nichangie upande wa wanamuziki ambao ndio wazalishaji wakuu wa bidhaa hii.Kiukweli wao ndio wamepoteza dira na kuzalisha bidhaa hafifu ambayo haitushawishi wateja.Tatizo siku hizi kwenye band hakuna wapangaji wa muziki ila tu mwenye sauti ndio hupanga muziki!Matokeo yake yy mwenyewe hajui kisha huyo huyo ndio apangie wengine!Utunzi,hapa ndio kwenye tatizo kila mtu ni mtunzi!Zamani kulikuwa na watunzi tena wengine hawjishughulishi kabisa na muziki lkn band/wanamuziki walitungiwa nyimbo na wao kuziimba tu.Lkn siku hizi ukiwa mwimbaji basi tayari una cheo cha kutunga!Matokeo yke mtu anajitungia tu!Kibaya zaidi hakuna wahariri wa hizo nyimbo!Tuna ushahidi wa nyimbo ambazo zilitungwa na watu wasiojulikana na zilibamba.Band zibadilike zifuate misingi na sheria za muziki

Comments