MKUTANO WA KWANZA WA VIONGOZI WA BENDI 2014 WAFANYIKA BASATA LEO

Mkutano wa kwanza wa viongozi wa bendi mwaka huu, uliofanyika katika ukumbi wa Basata Jumanne tarehe 25 March umekuwa na mengi mazuri. Kwanza wanamuziki walikumbushwa mengi ambayo yameshindikana kufanyika kwa kutokuweko na umoja wenye nguvu wa wanamuziki, hasa wa muziki ‘live’, hivyo kulipatikana azimio kuwa wanamuziki wahamasishane wenyewe kujiunga na vyama vya muziki. 
Maelezo pia yalitolewa kuhusu nafasi ya sanaa katika Katiba mpya na juhudi ambazo zimekwisha fanywa na jinsi zinavyohitaji umoja katika kipindi hiki cha Bunge la Katiba. Viongozi hawa hatimae walizungumzia changamoto mbalimbali ambazo zinaikumba tasnia hii, na kuamua kuanza kujipanga kupunguza matatizo yale ambayo yako katika uwezo wa bendi. Iliamuliwa kuweko na kikao kingine Jumanne ijayo kuanzia saa nne asubuhi palepale BASATA na kutafuta wajumbe wengine kutoka bendi ambazo hazikuhudhuria mkutano wa leo.







Comments