HARAKATI ZA WASANII KUPATA NAFASI KATIKA KATIBA MPYA—2



 Ili kuwezesha kufika Dodoma na kuwakilisha mapendekezo yaliyokusanywa na Mashirikisho, Mtandao wa Wanamuziki Tanzania (TAMUNET), waliwezesha idadi ya wasanii 12 kufika na kuishi Dodoma. Wasanii hao wakiwemo viongozi toka Mashirikisho wameza kufika Dodoma na kuanza kazi mara moja ya kukutana na Wabunge mbalimbali, na kufanya nao mikutano na mazungumzo ya papo kwa popa na kwa kweli mapokezi yamekuwa ya hali ya juu yanayoleta tumaini kubwa kwa  wote waliofika huku. Wasanii waliomo katika msafara huu muhimu kwa tasnia na Taifa ni



1.     Simon Mwakifwamba – Rais, Shirikisho la Filamu (TAFF)

2.     John Kitime – Mwenyekiti, Tanzania Musicians Network (TAMUNET)

3.     Bishop Hiluka – Katibu Mkuu, TAFF

4.     Yobnesh ‘Batuli’ Yusuph –Msanii/FilmProducer

5.     Samwel ‘Braton’ Mbwana –Tanzania Urban Music Association (TUMA)/Music Producer

6.     Paul ‘P Funk’ Matthysse – Mwenyekiti, Tanzania Producers Association/ Producer

7.     Kulwa ‘Dude’ Kikumba – Msanii/ Producer

8.     Abdul Salvador –Katibu Mkuu, Shirikisho la Muziki Tanzania (TMF)

9.     Adrian Nyangamale – Rais, _Shirikisho la Sanaa za Ufundi Tanzania

10. Mh. Paulynus Raymond Mtendah – Mbunge Bunge la katiba

11. Yvonne Cherie ‘Mona Lisa’ –Msanii

12. Seleman Hamisi- Producer toka Dodoma

13. Ernest Omalla – Mshauri wa TAFF na TAMUNET

Mara baada ya kufika Dodoma Mbunge wa Bunge la Katiba Mh. Maria Sarungi aliwezesha kufanyika kikao cha kwanza kati yake na wasanii ambapo pia Mh. Paul Makonda alikuweko. Mazungumzo yalifanyika ambapo msafara ukaweza kueleza mapendekezo yake kupitia mshauri mtaalam Ernest Omalla na mwanamuziki John Kitime. Mkutano huu wa saa mbili ulikuwa wenye matumaini makubwa.
Msafara ulitoka hapa na kwenda kwenye mkutano mwingine ambapo msafara tena ulitoa maelekezo yake kwa waheshimia Wabunge watatu, Mh Paul Mtanda, Mh.Livingstone na Mh Murtaza Mangungu, na tena mkutano huo ulikuwa ni mzuri wenye mafanikio mazuri sana. Mheshimiwa Mtanda aliahidi atajitahidi kukusanya wajumbe wa kamati ya Ustawi wa Jamii ili kuweza kupata uelewa wa maombi ya wasanii.




Kamati haikuishia hapo kwani jioni Mheshimiwa  Makonda aliiwezesha kundi hili kukutana na wabunge wengine wakiwemo  Mh. Ahmed Salum, Mh. William Mgeja na Mh. Mpina Mbunge wa Kisesa.



Katika hali ya kuonyesha kuwajali wasanii wabunge wa Dar es Salaam waliwafuata wasanii katika Lodge waliofikia na kuwasikiliza lile ambalo walikuwa wakilitaka. Mheshimiwa Idd Azan na Mh. Abbas Mtemvu waliwakilisha wabunge wa Dar es Salaam na kuwa na saa nzima ya kuwasikiliza wasanii hawa katika malengo yao mawili waliyotaka yaingie katika Katiba.

Comments