KIKAO CHA TATHMINI YA TANZANIA MUSIC AWARDS 2013 CHAFANYIKA BASATA


Tanzania Music Awards 2013, leo ilifanyiwa tathmini katika ukumbi wa BASATA. Muwakilishi wa katibu Mtendaji wa BASATA, Mama Shaluwa ndie aliye kuwa Mwenyekiti wa kikao hiki cha kufanya tathmini. Wajumbe mbalimbali walikuwemo katika kikao hiki wakiwemo watangazaji wanamuziki watendaji wa BASATA, Meneja wa brand ya Kilimanjaro Premium Lager, na wawakilishi wa kampuni ya Executive Solutions. Tathmini ilianza kwa Bwana George Kavishe kutoa taarifa ya mafanikio na changamoto mbalimbali zilizokuwepo katika kuendesha  TMA 2013, na ndipo michango mingi ya kuboresha Tuzo hizi ilitolewa.  TBL iliahidi kuboresha tuzo hizi kuanzia upande wa utafutaji wa nyimbo, kuboresha utafutaji wa washiriki wa Academy na utafutaji wa Majaji. Inategemewa kuwa TMA 2014 itakuwa bora zaidi mwaka huu.




Comments