MADANSA WATENGENEZA CHAMA CHAO


Madansa wa Tanzania ambao ni maarufu kwa jina la ‘ wacheza show’ hatimae wameweza kuunda chama chao Tanzania Dancers Association, ambacho si tu kina uongozi wa Kitaifa lakini pia tayari kina matawi ya kiwilaya. Jambo ambalo vyama vingi vya sanaa havijaweza kufikia.
Mwenyekiti wa Taifa wa Chama hiki ni Bi Husna Katibu wake akiwa ni dansa maarufu Chino Loketo.
Viongozi wa Taifa

Jumatatu hii chama hiki kilifanya mkutano mkubwa na kumkaribisha Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanamuziki kuwa mgeni rasmi wa mkutano wao huu mkubwa uliofanyika pale Garden Breeze Magomeni.
Pamoja na John Kitime pia walialikwa wanamuziki maarufu kama Waziri Ally wa Kilimanjaro Band, Nyosi El Saadat Rais wa FM Academia, Ally Chocky Mkurugenzi wa Extra Bongo, na Hussein Tendega maarufu kama Hussein Macheni.
Katika kikao hiki, Nyoshi alitoa mchango wake kwa chama wa shilingi laki moja, na Ally Choky aliahidi laki mbili, Hussein Macheni pia aliahidi laki mbili. Hussein Macheni amekuwa kiungo kikubwa kwa madansa hawa kwa kuwa wakati akiendesha bar maarufu kwa jina la Macheni madansa wengi walipitia katika ukumbi wake.
Mgeni rasmi aliwasifu madansa kwa kuanzisha chama chao, na pia alitoa msaada wa kuwaboreshea Katiba yao na kuwaahidi kuwaunganisha na vyama vingine vya madansa nje ya mipaka ya Tanzania.
Madansa walionyesha uwezo wao kwa kufanya show mbalimbali kama zinavyoonkana katika picha na video hapa chini


Nyoshi El Sadat

Ally Chocky


Waziri Ally


Hussein Macheni akihutubia

Comments