MASHINDANO YA KIGOLI WA TZ 2013 YATANGAZWA RASMI...KITIME MMOJA WA MAJAJI


Mashindano ya Kigoli wa TZ 2013 yaliyotayarishwa na mtangazaji maarufu Maimatha wa Jesse yametangazwa rasmi katika ukumbi wa The Olympia, paleeee Sinza Mori. Waandishi mbalimbali  walipata taarifa juu ya shindano hili litakalojumuisha mabinti wa kuanzia umri wa miaka 18 hadi 28, ambalo litazinduliwa rasmi tarehe 31 May, 2013 na kufikia kilele mwanzoni mwa mwezi July.
Majaji wa mashindano hayo ambayo pia yatashirikisha mabinti kutoka Morogoro na Tanga watakuwa Maimatha, John Kitime, na Musa wa Kitaa





Comments