PIGO KUBWA KWA MUZIKI WA TAARAB


Wiki hii imekuwa mbaya sana  kwa muziki wa Taarab. Katika wiki hii, Haji Mohamed Mkurugenzi wa East African Melody, kundi lililoanzia Zanzibar na kufikia kutikisa nchi za Afrika Mashariki, Kati na hata Uarabuni, alifariki kwa maradhi katika hospitali ya Muhimbili. Leo hii tumempoteza Bibi kipenzi Bi Kidude. Bwana Haji ambaye alikuwa na uwezo mkubwa wa kupiga kinanda chenye
BI KIDUDE

HAJI MOHAMED
scale za kizungu na kupiga kinanda kilichokuwa katika scale za Kiarabu, pia alikuwa muimbaji mahiri wa nyimbo za Kiswahili na Kiarabu. Na aliwahi kusema Bi Kidude alikuwa mmoja wa waalimu wake. Bi Kidude ambaye alikuwa akiweza kuimba Kiswahili na Kiarabu pia alikuwa mahiri aliyesema kuwa alikuwa anafuata nyayo za Siti Binti Sadi. Wawili hao mtu na mwanafunzi wake wametuacha wiki hii.
Mungu awalaze pema peponi

Comments