IRENE UWOYA, RAY, JB , KING MAJUTO NDANI YA RWANDA MOVIE AWARDS




 The Rwanda Movie Awards zilizofanyika Kigali Serena Hotel siku ya Jumapili iliyopita zilikuwa ni shughuli ya masaa matatu na nusu yenye shamra shamra za hali ya juu, zilizoongozwa na mtangazaji maarufu wa Radio Rwanda Tidjara Kabendera.
Irene Uwoya akiwakilisha
Shughuli nzima ilianza saa moja kamili usiku ambapo wapenzi wa filamu toka kila kona ya jiji la Kigali waliingia katika ukumbi wa Serena Hotel ili kuona kuzinduliwa kwa Rwanda Movie Awards. Nyota wa filamu kutoka Tanzania walikuwepo wakiwakilishwa na Irene Pankras Uwoya, Ray Kigosi na Jacobs Stephen, walioambatana na mchekeshaji maarufu King Majuto
King Majuto akiingia ukumbini
Tuzo zilitolewa kwa category mbalimbali ambazo zilifuata maamuzi ya majaji, na pia kulikuwa na kura kupitia internet ambazo zilizotoa ‘people's choice’. Kulikuweko na category kumi ikiwemo ya the Best Child actor. Tuzo zilikwenda kwa wafuatao;
Best film documentary: The impact of given a cow to the people of Rwanda by Ishmael Ntihabose.
Best short film: Kivuto
Best Actor: Munanura Habyalare
Best Actress: Fidelite Irakoze Sonia
Best Director: Muniru Habyakare
Up coming group/Dynamic awards: Happiness Games
People's Choice Actor: Denis Nsanzabaganwa
Best Female People's Choice: Marie France Niragire.
Best People's Movie: Ibanga
Young Best Actress: Esther Ngabire
 Kikundi cha Bibaho Film Actors, ndio kilichukua tuzo ya Best Actors' kwa mwaka 2012-2013. Mkurugenzi wa kundi hili Muniru Habyakare alichukua tuzo la Best Director na Best Film Actor of the year

Mmoja wa majaji  Kennedy Mazimpaka, akielezea kwanini ililazimika kuweko na majaji alisema katika kuchambua filamu ililazimika kuchambua kitaalamu script, kuangalia ubora wa sauti katika filamu na hata jinsi waigizaji walivyotimiza kazi yao, ila mambo mengine yalitegemea kura za wapenzi kupitia internet. Uwepo wa wasanii wetu wa Tanzania katika shughuli hiyo hakika ni ushahidi wa hatua kubwa waliyofikia katika tasnia ya filamu Afrika Mashariki

Comments