BREAKING NEWSSS--MSAMBAZAJI WA MUZIKI WA KIMATAIFA KUJA DAR ES SALAAM


TAARIFA NZURI NA MUHIMU kwa wanamuziki na ma Producer, na wenye label za muziki Tanzania, hususan Dar es Salaam.Mkurugenzi mtendaji CEO wa kampuni ya Africori, kampuni ambayo husambaza kazi kwa kupitia mitandao,(online digital distribution company) atakuweko hapa nchini kukutana na wale wenye nia ya kusambaziwa kazi zao kwa kutumia njia hiyo, ambayo itaweka muziki(audio na video) katika mtandao na kuweza kununuliwa na watu wote ulimwenguni na pia hata kuonekana na makampuni ya kimataifa yenye uwezo wa ununuzi wa haki za muziki wa kwenye simu(ringtones), na kukuachia asilimia kubwa ya mauzo hayo. Kwa wale wenye nia ya kuonana na mfanyabiashara huyu, atafika nchini Jumanne tarehe 12 March na kuondoka Alhamisi tarehe 14, wenye nia ya kuonana nae na wenye kazi za kuuza tafadhali nitaarifuni kupitia email jkitime@gmail.com

Comments