Monalisa na Natasha katika FILAMONATA CHA TIMES FM WATIMIZA MWAKA 1

Kipindi cha Filamonata kinachorushwa na Times FM kimetimiza mwaka mmoja. Kipindi hiki cha kipekee ambacho huongelea mambo ya filamu za hapa nchini na duniani kwa ujumla kimepata umaarufu mkubwa kwa kuwa sehemu ambayo unaweza kupata ukweli kuhusu mambo ya filamu Tanzania. Kipindi kinaendeshwa na wasanii wawili mahiri katika tasnia ya filamu, Susan Lwewis aka Natasha na binti yake Yvonne Ngatuka aka Monalisa. Katika kusherehekea mwaka moja wasanii kadhaa walikaribishwa kama wanavyoonekana katika picha. John Kitime nae aliialikwa na kuja na gitaa lake na kupiga nyimbo kadhaa za zamani.

















Comments