Lady In Red 2013 Upgraded yatambulishwa rasmi


Bi Asya Khamsini









Lady In Red 2013 Upgraded, leo imetambulishwa rasmi kwa vyombo vya habari katika ukumbi wa  Nyumbani Lounge. Mkurugenzi Mtendaji wa Lady In Red Bi Asya Khamsini alitambulisha wafadhili kadhaa waliokuwepo katika ukumbi huo, pia models na Designers watakao shiriki katika Fashion show hiyo itakayofanyika tarehe 9 February 2013 katika hotel ya Serena.
Kwa maelezo ya Asya, show hiyo itakuwa na Designers wengi wapya na wachache wakongwe, hii ni makusudi ili kuweza kuwaingiza designers wapya katika ulimwengu wa designers. Katika siku hiyo pia kutakuweko na mnada wa kukusanya fedha kwa ajili ya kuendelea kituo cha waathirika wa madawa ya kulevya kilichoko Rufiji.

Comments