WASANII WALETA MTAFARUKU MKUBWA KWENYE MKUTANO NA TRA..


Semina ya TRA ya URASIMISHAJI WA TASNIA YA MUZIKI NA FILAMU, imeisha kwa kusambaratika bila kuagana rasmi kutokana na wasanii kuja juu na kuuliza maswali ambayo majibu yake hayakuwaridhisha wasanii.Hivyo kuzuka mtaafaruku mkubwa katika ukumbi.
Semina hiyo ambayo ilitangazwa kuwa ingekuwepo katika ukumbi mkubwa wa Jumba la Makumbusho ya Taifa katikati ya Jiji la Dar es salaam ilikuwa imepangwa ianze saa nne lakini ilichelewa na kuanza saa 5. Wasanii mbalimbali, vijana na wazee wa filamu na muziki wakisindikizwa na viongozi wa vyama na Mashirikisho yao walikuwemo. Kwa upande wa serikali kulikuweko na Maafisa kutoka Ukurugenzi wa Utamaduni, BASATA, COSOTA, Bodi ya Filamu wakiongozwa na TRA  ambao ndio walikuwa wasemaji wakuu. Semina ilianza kwa maelekezo kuhusu nini kitakachofanyika ili kuanza kuhakikisha stika za TRA zimebandikwa kwenye kila kazi ya sanaa(CD,DVD,Kanda na kadhalika). Kwa maelezo  ya muwezeshaji hili lingeleta faida kwa kulinda haki za wasanii. Iliilezwa kuwa taratibu hizi zitaanza Januari 2013 kwa kazi zote mpya na kwa kazi ambazo ziko dukani zitatakiwa zote kuwa na stika hizo kufikia July 2013. Kazi zote  zilizotakiwa kusambazwa nchini kuanzia sasa, zingelazimika kupitia COSOTA, BASATA, na Bodi ya filamu kabla ya kuruhusiwa kupewa stika. COSOTA  itakuwa ikihakikisha uhalali wa kazi, BASATA na Bodi ya filamu kuhakiki maadili ya kazi husika.Wasanii waliporuhusiwa kuuliza maswali walihoji kwanza kuhusu zilipofikia Kanuni za sheria ya filamu, kwani ni muhimu katika taratibu hizi, na pia wasanii walihoji COSOTA  ina muwakilisha nani?, kwani ilikwishabadilika kinyemela kutoka kuwa Chama cha wenye Hakimiliki na kugeuzwa kuwa kitengo cha serikali, na kuanzia 2007 hakijawahi kuitisha mkutano na wadau, japo kinaendelea kukusanya fedha za wadau. Wasanii pia waliuliza TRA kwanini inadai inawalinda wasanii wakati ni wazi katika hili kazi yake itakuwa ni kukusanya kodi kutoka kwa wasambazaji, jambo ambalo halina tija yoyote kwa wasanii binafsi. Majibu yaliyotolewa yalileta mvurugano kiasi cha kusababisha viongozi wote kuondoka kimyakimya kupitia mlango wa nyuma na kuwaacha wasanii wakiendelea na kikao kisicho rasmi ambacho kilihamia nje ya  kufikia kutengeneza kamati ambayo itatayarisha mkutano mkubwa wa wasanii wote wa muziki na filamu kutoa tamko la pamoja.Tatizo la taratibu hizi zinazotaka kuanzishwa hapa nchini ni mpya kabisa hazijawahi kufanyika nchi nyingine yoyote kwa mtindo huu, haieleweki kwanini serikali inataka kugundua njia ya kibongobongo ya kulinda kazi za wasanii, wakati duniani kote taratibu zinafahamika, hii inaleta picha kuwa serikali inahitaji tu kodi kutoka kwa wasanii lakini haina mpango wa dhati kuhusu wasanii.


Maswaliiii


Wasanii nje ya ukumbi mkutano ukiwa unaendelea ndani






Mkutano wahamia nje






Comments

Kaka KITIME, hili ndiyo tatizo la mabadiliko ya Ghafla ya kutoka ngazi ya Juu kwenda Chini. na wala sio kutoka chini kwenda ngazi za juu!
wamekurupuka!