WASANII IRINGA WAJA NA WIMBO-IRINGA BILA UKIMWI INAWEZEKANA



MBUNGE wa Viti Maalumu wa Chama cha Mapinduzi, mkoa wa Iringa, Ritha Kabati, ameshirikiana na washindi 20 wa ‘Kabati Katiba Star Search’ kutoa kibao kipya cha Muziki wa Bongo Flava kiitwacho ‘Iringa Bila Ukimwi Inawezakana’, .
Kibao hicho alichorekodi na wasanii chipukizi wa muziki wa kizazi kipya walioibuka washindi wa shindano hilo la kusaka vipaji, umerekodiwa katika studio za Top Magic Sound chini ya mtayarishaji wake mahiri Ecko
Wimbo huo ni harakati za Mheshimiwa Mbunge Kabati alizozianzisha katika kuwakomboa vijana katika majanga na makundi hatarishi kama ya uvutaji wa bangi, ngono zembe zinazochangia maambukizi ya ukimwi – ugonjwa ambao kwa mujibu wa takwimu za mkoa huu unaongoza kwa maambukizi mapya.
Akiuzungumzia wimbo huo,Mh. Kabati amesema ana imani ujumbe uliomo utaifanya jamii kubadilika na hatimae kupunguza kasi ya maambukizi ya virusi vya ukimwi mkoani iringa na taifa kwa ukjumla.
WIMBO-IRINGA BILA UKIMWI INAWEZEKANA
ARTIST-KABATI ALL STARS
STUDIO-TOP MAGIC SOUND IRINGA
PRODUCER-ECKO

Comments