Tanzania Film Training Center..Yafanya mahafali ya kwanza

Tanzania Film Training Center leo imeanzisha rasmi mapinduzi makubwa kwenye tasnia ya filamu, mapinduzi ambayo mtu yoyote mwenye mapenzi mema na tasnia nzima ya burudani Tanzania atafurahia na kuyaombea yaendelee na kuenea kwenye fani nyingine zote. Leo wahitimu zaidi ya 30 wamehitimu masomo ya fani mbalimbali za utengenezaji wa filamu. Sherehe ya leo ilifana sana na mgeni wa heshima alikuwa Mtendaji Mkuu wa Tanzania Film Board Mama Fisoo. Kati ya wasanii walionyesha njia ni msanii maarufu Zawadi ambaye licha ya kuwa ameshakuwa katika tasnia kwa miaka mingi tokea enzi za mwanzo za Kaole, aliona ni vema akiingia darasani na kupata uelewa wa fani kupitia masomo ya chuoni  
Wahitimu


High Table Katibu Mkuu TAFF, Rais TAFF, Mkuu wa Chuo Tanzania Film Training Center, Mtendaji Mkuu Tanzania Film  Board









Picha ya pamoja

Ufunguzi wa dansi rasmi



Zawadi na familia yake


Comments