MA'LEGEND' WA KIBONGOBONGO



Siku hizi imeanza kuwa kawaida wasanii nchini kuitwa au kujiita ‘Legends’. Je, neno hili maana yake nini? Neno hili limetokana na neno la Kilatini ‘legenda’ ambalo maana yake ni ‘Mambo muhimu ya kusomwa’. Hapo awali mambo hayo yalikuwa ni hadithi na vitendo vya binadamu, vya kusikia, kuhisi na hata kutungwa ambavyo vilionekana vilifanywa katika historia ya ulimwengu. Katika ‘legends’ kulikuweko na aina ya ushahidi unaoweza kutetea maelezo husika.
Katika siku za karibuni, mtu ambaye ameweza kuleta mapinduzi katika fani husika pia ameweza kuitwa ‘Legend’, kwa mfano Steve Jobs aliyeweza kuleta mabadiliko na mapinduzi makubwa katika teknolojia iliyotuletea  iPad, iMac, iPhone na kadhalika. Ni kitu kinachochekesha wakati msanii wa Bongo aliyebobea kwa kurudia mitindo na Beat walioanzisha wenzie( Congo, Nigeria, South Africa), eti nae anatangazwa kwenye vyombo vya habari kuwa ni ‘legend’ au pengine kwa ajili ya umri wake tu kuwa mkubwa tunaambiwa ni ‘legend’. Hi si sawa, ‘ulegend’ unatokana na mambo anayofanya mtu yanayoleta mchango au mabadiliko katika historia ya fani ya muhusika.

Comments