MUIMBAJI MARIAM KHAMIS WA TOT TAARAB AFARIKI DUNIA

-->

MWIMBAJI nyota wa taarab nchini, Mariam Khamis aliyekuwa katika kikundi cha TOT Taarab, amefariki dunia katika hospitali ya Muhimbili baada ya kujifungua usiku wa leo. Mariam alijiunga na TOT akitokea katika kundi la  Five Stars Modern Taarab.
Mariam, ambaye aliwahi kutamba kwa kibao chake cha ‘Paka mapepe’,  mbali na kuimbia kundi la Five Stars, Mariam pia aliwahi kung’ara alipokuwa katika vikundi vya East African Melody na Zanzibar Stars.Baadhi ya vibao alivyotamba navyo katika vikundi hivyo ni pamoja na ‘Huliwezi bifu’, ‘Raha ya mapenzi’ na ‘Ndo basi tena’.
Mungu ailaze pema roho ya Mariam

Comments