MTANGAZAJI LULU OSCAR AFARIKI DUNIA


Lulu Oscar binti mchangamfu ambaye kwa karibuni alikuwa mtangazaji wa SIBUKA TV akiendesha kipindi cha Pepeta Afrika, ambacho alikifanya mara nyingi akiwa na mwanamuziki Hamza Kalala, na ameweza kuwahoji wanamuziki wengi sana wa aina zote za muziki, amefariki dunia usiku wa kuamkia leo. Lulu alikuwa anaumwa siku za karibuni, na alikuwa amelazwa hospitali.
Lulu alikuwa mchangamfu na mcheshi mwenye kupenda sana utani, nilimfahamu awali akiwa mtangazaji katika radio moja kule Njombe, ambapo hatimae aliamua kuhamia Dar es Salaam kutafuta maisha na akapata kazi Sibuka TV.
Mungu Amlaze peponi pema Amen

Comments