MSANII WA FILAMU JOHN MAGANGA AFARIKI DUNIA

RIP JOHN MAGANGA
Kwa mara nyingine tena wiki hii tasnia ya filamu imepoteza msanii mwingine baada tu ya kumaliza mazishi ya Mlopelo. Msanii John Maganga amefariki katika hospitali ya Muhimbili.  Taratibu za mazishi bado zinafanyika.
Ni hivi karibuni tu msanii huyu alisema kuwa amefungua Kampuni yake ijulikanayo kwa jina la Jom Entertainment Co. Ltd, pia akaeleza kuwa alianza kuona kipaji chake tangia mwaka 2001 alipokuwa akifundishwa na msanii nguli wa filamu nchini Ndumbago Misayo 'Thea' ambaye alikuwa mwalimu wake wa maigizo wakati wapo kanisani pale Mwananyamala, baada ya hapo filamu ya kwanza iliyokwenda kwa jina la Miracle of Love  ambayo ilifanya vizuri sana katika kumtambulisha kisanaa nchini. Mwaka 2008 alishauriwa na ndugu yake Deogratias Shija kufungua kampuni yake kwa ajili ya kuendeleza fani ya filamu, kazi ambazo ziko tayari ni Beautfuls aliyowashilikisha wasanii kama Aunt Ezekier, Haji Salumu 'MBoto' na wengine wengi
Mungu aiweke pema roho ya msanii huyu ambaye ameondoka wakati anaanza kuchipua.

Comments

Anonymous said…
RIP JOHN MAGANGA