MARIAM KHAMIS AZIKWA NA UMATI MKUBWA

 
Kwa muda barabara ya Magomeni kwenda Sinza kupitia Tandale eneo la Somanga, Magomeni makuti, ililazimika kufungwa kwa magari ili kupisha umati mkubwa wa watu waliokuwa wakisindikiza mwili wa Mariam Khamis kwenda katika mahala pake pa mwisho duniani. Mariam ambaye alikuwa muimbaji wa bendi ya TOT Taarab alijulikana sana kwa wimbo wake 'Paka Mapepe' alipoteza uhai wake jana katika hospitali ya Muhimbili, kutokana na matatizo baada ya kujifungua. Ukubwa wa umati ule ni kielelezo kikubwa kuwa marehemu alipendwa na watu. Mungu ailaze Roho yake pema peponi Amin










Comments