LADY JAY DEE KUJA NA KIPINDI KIPYA CHA KWENYE TV


Mwanamuziki  muimbaji mahiri Judith Wambura (kulia) maarufu kwa jina la Lady Jay Dee ametambulisha rasmi  kipindi chake kipya cha luninga kitakachoitwa ‘Diary ya Lady Jay Dee’.
Mkuu wa Vipindi wa East Africa TV Bi. Lydia Igarabuza(kushoto), akiwa na Lady Jay Dee
Jay Dee amesema madhumuni ya kipindi hicho ni kuleta burudani tofauti kwa wapenzi wa muziki wake, na muziki wa kizazi kipya kwa ujumla, vilevile kitatoa fundisho na changamoto kwa wasanii chipukizi kujua wasanii wakongwe wamepitia katika vikwazo gani.
 Kipindi hicho kitakuwa hewani East africa Tv-Channel 5, Jumapili saa 3 usiku kuanzia Novemba 18.2012

Comments