WASANII WA ARUSHA WALAANI KUDHARAULIWA

TATIZO LA WASANII KUDHARAULIWA NA MAAFISA UTAMADUNI NI LA KAWAIDA SANA HAPA NCHINI SIKU HIZI, WENGI BADO TUNAKUMBUKA AFISA UTAMADUNI MUSOMA ALIPOAMRISHA WASANII KUWEKWA NDANI KWA SABABU AMBAZO MPAKA LEO HAZIJAJULIKANA. JUZI AFISA UTAMADUNI MMOJA HAPA DAR ALIKUWA AKIJITAHIDI KUZUIA TAMASHA LA UTAMADUNI LISIFANYIKE, SASA SIJUI YEYE KAZI YAKE INA MAANA GANI KAMA HAKUNA MAONYESHO YA UTAMADUNI. KWA SISI WASANII WENGINE AMBAO TULIWAHI KUISHI KATIKA SERIKALI AMBAPO MAAFISA UTAMADUNI WALIKUWA CHINI YA WIZARA YA UTAMADUNI, NA KILA AFISA ALIJITAHIDI WASANII WAKE WAWE BORA ZAIDI, KWA KUWA MAAFISA UTAMADUNI WALIKUWA WOTE WAKIFUATA MWONGOZO MMOJA WA WIZARA YA UTAMADUNI MATATIZO KAMA HAYA YALIKUWA MACHACHE, KIUKWELI ILIKUWA MARA NYINGINE NI KERO KWANI KAMA KULIKUWA NA SHUGHULI YA NYUMBANI WASANII WA NYUMBANI WALINYIMWA HATA KIBALI CHA KUTOKA NJE YA MKOA KWANI WAO WALIKUWA NDIO WENYEJI WA SHUGHULI. INASIKITISHA SANA KWANI ARUSHA HIYO NDIO ILIKUWA KATI YA KURUGENZI YA KWANZA HATA KUWA NA BENDI YA ILIYOMILIKIWA NA KURUGENZI YA ARUSHA. ARUSHA KILIKUWA NDIO KITUO KIKUBWA CHA WANAMUZIKI NA BENDI MAARUFU NYINGI ZILIANZIA AU KUHAMIA ARUSHA.......

 Wasanii wa muziki wa kizazi kipya na vikundi mbalimbali vya maigizo mkoani Arusha wamewataka  viongozi wa serikali kutowadharau na kuwashirikisha kikamilifu katika shughuli mbalimbali za maendeleo jijini hapa

Hali hiyo imetokea wakati zikiwa zimebaki siku chache ili kufanyika uzinduzi rasmi wa Jiji la Arusha baada ya wasanii hao kudai kutoshirikisha kwa lolote .

Akizungumza kwa niaba ya wasanii wenzake msanii wa muziki wa kizazi kipya Nakaaya Sumari alisema kuwa wameshangaa sana kusikia kuwa msanii kutoka dar es salaam Diamond Platnum atakuja kutumbuiza  ilihali wao wapo na hawana taarifa yeyote.

Nakaaya alisema kuwa hawana tatizo na Nasibu Abdul (Diamond) ambaye amealikwa kuja kusherehesha uzinduzi huo ila walichokiona ni dharau kutoka kwa afisa Utamaduni wa manispaa kwa kutoonyesha ushirikiano na  badala yake wamepewa taarifa ya kufanya kitu juuya uzinduzi huo kama zima moto jana usiku baada ya wao kuulizia.

“Tumeshanga sana hii ni dharau wasanii wa arusha hatuheshimiki kabisa na tumeuliza ndo tunaambiwa eti tuandae kitu kwa ajili ya uzinduzi dah yani inakatisha tamaa sana alafu afisa utamaduni mwenyewe anatuona anatupotezea”alisema nakaaya

 Hata hivyo Nakaaya alimpongeza  Meya wa jiji la Arusha Gaudence Lyimo kwa kutoa ushirikiano wake kwao na kuahidi kushirikiana nao kwa madai ya kilichofanyika ni makosa ya kibinadamu.

Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha wasanii mkoa wa arusha Hussein Sechonge alikemea vikali tabia hiyo kwa kuwa wasanii wana mchango mkubwa wa kufikisha ujumbe na kuwataka viongozi kuwa wazalendo.


Aidha walimtaka afisa utamadumi manispaa  Juma Sule kutoa ushirikiano kwa wasanii wa hapa kwa kuwa wao ndio wanajua kila kitu kuhusu manispaa na sio Diamond.

”tunamshangaa sana hapa kuna wasanii 70 sasa nashangaa kwenye mwenge aliletwa Juma Nature wakati wao wapo hapa na hawafahaamu kitu chochote sio vizuri”alisema Sechonge.

Hadi jamii blog inaondoka  katika ofisi za manispaa  wasanii hao walikuwa  nje ya ofisi ya meya wakisubiri kujadiliana namna ya kufanya na kumaliza tofauti hiyo. HABARI NA PICHA TOKA http://pamelamollel.wordpress.com/

Comments