SHINDANO LA KUSAKA VIPAJI LA KABATI KATIBA STAR SEARCH awamu ya pili 27 Oktoba




Jumamosi tarehe 13 Oktoba katika ukumbi wa Welfare Center, mambo makubwa mawili yalifanyika, kwanza vijana wengi walioshiriki na wale waliokuja kufuatia Kabati Katiba Star Search walipata elimu nzuri ya Katiba ya Tanzania. Na pili ilikuwa burudani kwa kwenda mbele kutoka kwa vijana walioshiriki Star Search kuonyesha vipaji vyao. Vijana 150 waliweza kujitokeza kuonekana mbele ya jopo la majaji
majaji  Eddo Bashir (Ebony Fm), Temmy Mahondo (Country Fm), Dj Ammy Yeyo (Country Fm ), Agnes Anderson (Ebony Fm) na Dj Muba wa (Ebony Fm) . Mchujo uiofanyika baada ya hapo uliwezesha vijana 20 kuingia katika Top Twenty ya mpambano huo. Tarehe 27 Oktoba ndipo itakapoingia awamu ya pili ya shindano hili na Top Ten kupatikana.

Comments