MOHAMED IDD CONTROL AFARIKI DUNIA


TANZIA, Mpiga gitaa mahiri MOHAMED IDD aka "CONTROL" amefariki dunia leo alfajiri. Wakati wa uhai wake marehemu amewahi kupigia bendi kadhaa zikiwemo Double O ya King Kiki,  National Panasonic, Mlimani Park, OTTU na alienda kufanya kazi Uarabuni na  Zanzibar Sound ya Asia Darwesh. Baada ya kukaa Uarabuni kwa muda aliamua kurejea bendi yake ya zamani ya Sikinde. Miongoni mwa vibao vilimpatia umaarufu ni pamoja na wimbo Gloria wa OTTU ambao alipiga solo. R.I.P IDD CONTROL

Comments