TWANGA PEPETA ZIARANI IRINGA NA MBEYA


Bendi maarufu ya African Stars Band maarufu kama Twanga Pepeta itakuwa na ziara ya maonyesho ya nguvu katika mikoa ya Iringa na Mbeya. Tarehe 14-09-2012 siku ya Ijumaa katika Twanga itakuwa katika ukumbi wa Highland.
Kesho yake siku ya Jumamosi tarehe 15-09-2012  watakuwa Jijini Mbeya ndani ya City Pub na siku ya Jumapili tarehe 16-09-2012 watafanya Bonanza maalum kwa ajili ya wakazi wa Jiji la Mbeya na maeneo ya jirani.
Bendi inataraji kuondoka Dar es Salaam mara baada ya kumalizika kwa onyesho la kila siku ya Alhamisi tarehe 13-09-2012 litakalofanyika Club Maisha Oysterbay.
Twanga Pepeta itakapokuwa katika ziara, itamtambulisha mwimbaji wao mpya Kalala Jr aliyerejea hivi karibuni kutoka katika Bendi  ya Mapacha Watatu. Sambamba na utambulisho huo pia itatambulisha nyimbo zao mpya za “Ngumu Kumeza” ilyotungwa na  Mirinda Nyeusi, huyu ni mwanamuziki aliyehamia karibuni kutoka Mashujaa Band, “Nyumbani ni Nyumbani” uliyotungwa na Kalala Jr, “Walimwengu” iliyotungwa na Jumanne Said  na ” Mapambano ya Kipato” uliyotungwa na Kocha wa Dunia, Mwinjuma Muumini.
Mara baada ya kurejea jijini, Twanga Pepeta itaendelea kufanya maonyesho yake kama kawaida Jijini Dar es salaam katika kumbi za Club Billicanas siku ya Jumatano, New Club Maisha siku ya Alhamisi, Free Time Resort Ukonga Banana, Mango Garden siku ya jumamosi na Jumapili mchana Leaders Club na usiku Mzalendo Pub.




Comments