Kofi Olomide atembeza ngumi, apewa kifungo

Mwanamuziki Antoine Christophe Agbepa Mumba maarufu kama  Koffi Olomide, ambaye karibuni katoka kwenye mashtaka ya kubaka huko Ufaransa, amepewa kifungo cha nje cha miezi mitatu kwa kumjeruhi producer wake baada ya ugomvi uliotokea kati ya hao wawili kwenye hoteli moja mjini Kinshasa.
Mwezi Februari katika jiji la Paris Ufaransa, wacheza show wake watatu walimfungulia mashtaka ya kuwabaka na kuwafungia ndani kinyume cha sheria, Kofi alikana haya mashtaka na kurudi zake Kinshasa.
Hili jipya limetokea baada ya Kofi kukutana uso kwa uso na Producer huyo Diego Lubaki anaejulikana zaidi kama Diego Music, na Kofi kuanza kumdai producer huyo fedha ambazo alimlipa watengeneza video lakini kazi hiyo haikufanyika.
Ngumi zikaanza kurushwa na mabaunsa kadhaa walilazimika kuamua tifu hilo, na Kofi akawekwa chini ya ulinzi. Ingawaje Lubaki baadae alitaka kufuta mashtaka, Hakimu aliamua kuendelea na kesi. Kofi akapatikana na hatia ya kumjeruhi Lubasi lakini mashtaka yaliyoambatana ya kuharibu mali ya hoteli(mlango mmoja ulivunjwa) yalifutwa na hakimu. Kofi alifika mahakamani na wanasheria kumi.
Katika kesi yake ya kubaka wanasheria wa Kofi walisema masteji show waliitunga ili wapate vibali vya kuishi Ufaransa.

Comments