Alphabeta Music Centre


Mark Manji amekuwa mpenzi wa muziki katika maisha yake yote na baada ya kustaafu kazi akaona ni heri afanya kile kitu ambacho amekuwa akikipenda katika maisha yake yote nacho ni muziki. Lakini si kwa kupiga muziki maana alishwa wahi kupiga muziki katika ujana wake, na hata kuwa na bendi na akajikuta akiangushwa na matukio. Aliwahi kununua vyombo vya bendi kutoka kwa Marealle wa Seview na kupiga muziki kwa muda mfupi, lakini akawa amepata kazi nje ya nchi akamrudishia tena vifaa hivyo bwana Marealle, baadae alipopata nafasi ya kununua vyombo akawa ananunua vichache vichache na hatimae kuwa na vifaa vya kutosha bendi. Karama Malegesu na vijana wenzie waliweza kumshawishi Manji kuanzisha bendi naye akaiita   Chikoike Sound(jina lililotokana na kuunganisha majina ya wanawe), bendi ilianza 1994, kati ya wanamuziki waliopitia bendi hiyo ni waimbaji Banza stone na Juma Malembeka. Kwenye mwaka 1999 baadhi ya wanamuziki wakamuibia vyombo vyake fulani, akaamua kufungia vyombo vyake, na hatimae baada ya kustaafu akaamua kufungua kituo cha kufundishia muziki.

Mark Manji









Kituo hiki kiko Tabata Liwiti karibu kabisa na kituo cha posta  Tabata. Kituo hiki ambacho kina waalimu wenye uzoefu wa miaka mingi hakina wanafunzi wengi hivyo kila mwanafunzi kupata nafasi ya kufundishwa vema, kina vifaa bora vya kisasa na pia kuna studio nzuri ya kurekodi iliyoko katika maeneo ya kituo.

Comments

Unknown said…
Hili ni wazo zuri sana Mr. Mark, ninaamini huu ni mwanzo mpya wa juhudi za kufanya muziki wa Tanzania ujitangaze kimataifa kwa kuwa na wanamuziki wenye ufahamu na muziki. Hongera sana sana.